West Ham kumnasa Maiga
Monday, 16 July 2012 10:39   

Klabu ya West Ham ya ligi kuu nchini England ipo katika hatua za mwisho kumnasa mshambuliaji Modibo Maiga kwa pauni milioni 4 kutoka Sochaux.

Maiga raia wa Mali alikaribia kujiunga na Newcastle january mwaka huu kabla ya dili hilo kuharibika kutokana na mshambuliaji huyo kugundulika ana majeraha ya goti.

Sam Allardyce ambaye ni kocha wa West Ham yupo katika harakati za kuimarisha safu yake ya ushambuliaji kabla ya msimu ujao kuanza.

Kocha huyo pia amekuwa akiwawinda mshambuliaji kutoka Norwich, Grant Holt na Yannick Sagbo kutoka klabu ya Evian.

AddThis Social Bookmark Button

 

Tuma maoni

Maoni yenye kukera, kutukana na kuvunja sheria za nchi yatafutwa

:D:lol::-);-)8):-|:-*:oops::sad::cry::o:-?:-x:eek::zzz:P:roll::sigh:
Bold Italic Underlined List Quote