Sunday 05th of September 2010
|
Topland, Shoko wang'ara Pool |
|
|
|
|
Written by Erasto Stanslaus
|
|
Saturday, 24 July 2010 15:42 |
|
Na Erasto Stanslaus
TIMU za Topland na Shoko zimeonesha matumaini ya kutinga katika hatua ya robo fainali ya michuano ya Safari Lager Pool Championship ngazi ya mkoa wa Kinondoni.
Michuano hiyo ambayo ilianza Julai 22 katika mikoa ya Ilala, Kinondoni, Temeke, Moro na Kagera, ambapo kwa Kinondoni inachezwa katika Bar ya Meeda, Sinza.
Shoko hadi sasa wanaongoza katika kundi A baada ya kushinda michezo yake miwili iliyocheza kati ya Meeda na Bahama Mama, wakati nafasi ya pili katika kundi hilo inashikwa na Meeda iliyotandika Jaba.
Katika kundi B, timu inayoongoza ni Topland iliyozichapa timu za Vatcan na Madrid katika michezo yao ya juzi na jana na Vatcan inashika nafasi ya pili katika kundi hilo baada ya kuifunga 4ways.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Chama cha Pool wilaya ya Kinondoni (KIPA), Zahor Lijalu, leo kwa Kinondoni watakuwa wamepata timu zitakazoingia hatua ya robo fainali zitakazopigwa Agosti 6 na nusu fainali itachezwa Agosti 7 na fainali itakuwa sikukuu ya nanenane.
Mashindano hayo ya mkoa yatatoa timu ya mkoa huo ambao itashiriki mashindano ya Safari lager Pool ngazi ya Taifa yatakayofanyika Septemba 15 hadi 19 mkoani Arusha. |
Powered by Business Times Ltd
Valid XHTML and CSS.