Sunday 05th of September 2010

Home
Habari za Michezo
Tegete aipa raha Yanga
Monday, 23 August 2010 06:00

Na Flora Amon, Dodoma

YANGA, jana iliichapa Polisi Dodoma bao 1-0 katika mechi ya kwanza ya Ligi Kuu soka Bara, iliyochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri, mjini Dodoma.

Mabingwa hao wa Ngao ya Hisani, walianza mchezo kwa kasi na kuliandama lango la wapinzani wao, lakini washambuliaji wake, Yahaya Tumbo, Jerry Tegete na Nsa Job, hawakuwa makini kupachika mabao mapema.

Read more...
 
Simba yaanza kishindo
Monday, 23 August 2010 05:59

Na Julius Kihampa

MABAO mawili ya mlinzi Ameir Maftah yalitosha kuipa Simba ushindi wa mabao 2-0 katika mchezo wake wa fungua pazia wa Ligi Kuu ya Vodacom nchini dhidi ya African Lyon jana.

Simba iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 katika mchezo huo uliopigwa katika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam ukiwa ni mchezo wa kwanza kwa timu zote mbili.

Read more...
 
Arsenal yafanya mauaji England
Monday, 23 August 2010 05:56

LONDON, England

ARSENAL jana ilifanya kufuru kwa kuilaza timu mpya iliyopanda daraja msimu huu, Blackpool mabao 6-0 katika mechi ya Ligi Kuu  England iliyochezwa Uwanja wa Emirates.

Timu hiyo imetoa kipigo kama ilivyofanya Chelsea iliyoichapa WestBwomwich katika mechi ya ufunguzi mwishoni mwa wiki iliyopita.

Read more...
 
Maligo wa Yanga afariki dunia
Monday, 23 August 2010 05:58

Na JUlius Kihampa

ALIYEKUWA mgombea wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti klabu ya Yanga, Costantine Maligo amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Maligo ambaye alikuwa ni miongoni mwa wagombea hao wa Yanga katika Uchaguzi Mkuu hivi karibuni alifariki jana saa 1 asubuhi.

Kwa mujibu wa ndugu wa malingo lianza kuumwa wiki mbili zilizopita akisumbuliwa na ugonjwa wa moyo  na kupooza ambapo alikimbizwa katika hospitali ya moyo ya Tumaini kabla ya kuhamishiwa Muhimbili ambako mauti yalipomkuta.

Read more...
 
Si muungwana
Monday, 23 August 2010 05:54

*Wenger amshutumu Scholes

LONDON, Uingereza

ARSENE Wenger, amemshutumu mchezaji wa Manchester United, Paul Scholes, kwa kumwita 'mchafu'.

Kocha huyo wa Arsenal, amedai mkongwe huyo wa United, ana upungufu mwingi na kusisitiza "samahani, kwangu mimi, yule si mchezaji muungwana."

Read more...
 
« StartPrev12345678910NextEnd »

Page 4 of 52

Swali la Leo

"Kitendo cha mabondia wa ngumi za ridhaa kususia mashindano kutokana na kutopatiwa chakura na nauli, ni maamuzi sahihi kwa maslahi ya Taifa letu?"
 

Who's Online

We have 7 guests online

Login Form




Powered by Business Times Ltd Valid XHTML and CSS.