Sunday 05th of September 2010

Home
Habari za Michezo
Simba kazi yaanza.
Monday, 30 August 2010 05:49

 
Simba yaanza kazi upya
Monday, 30 August 2010 05:48

Azam wamwamsha Phiri

Na Erasto Stanslaus

UBORA wa kikosi cha Azam FC, kimemfanya Kocha Mkuu wa timu ya Simba, Patrick Phiri kuamka na kukiandaa kikosi chake kwa ajili ya mchezo wao wa pili wa Ligi Kuu Bara utakaopigwa Septemba 11.

Phiri ambaye alichelewa kujiunga na timu hiyo katika maandalizi yake, kutokana na matatizo nyumbani kwao Zambia, ameamua kuanza kazi ya kukinoa kikosi hicho kutokana na mchezo wake dhidi ya Azam.

Miamba hiyo ambayo kila moja inapointi tatu baada ya kushinda michezo yao ya kufungua dimba kwa ushindi wa mabao 2-0, Simba ilinyuka African Lyon na Azam ikaichapa AFC Arusha.

Read more...
 
JKT yazidi kung'ara Ligi Kuu
Monday, 30 August 2010 05:46

Na Daudi Magera, Mwanza

TIMU ya Maafande wa JKT Ruvu wameendeleza ushindi wa ugenini baada ya kuinyuka Toto African bao 2-1 katika mchezo uliochezwa jana katika Uwanja wa CCM, Kirumba mjini hapa.

Bao la Pius Kisambare lililofungwa dakika ya 40, akitumia vizuri makosa ya kipa wa Toto, Husein Tade kutegeana na mabeki wake, liliifanya JKT kuondoka na pointi sita Kanda ya Ziwa baada ya kuitandika Kagera katika mchezo wao wa kwanza.

Read more...
 
Simba,Yanga, TFF, Serikali ngoma nzito
Monday, 30 August 2010 05:47

Na Winfrida Ngonyani

KLABU kongwe nchini za Simba na Yanga, bado zimeendelea kuvutana na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo, juu ya mapato ya Uwanja wa Taifa.

Klabu hizo sambamba na TFF na Wizara, wamekuwa na kikao cha muda mrefu wakijadili mapato ya mgao wa mchezo wao wa Ngao ya Jamii ikiwa pamoja na maombi ya kutumia uwanja wa Taifa katika michezo yao baada ya uwanja wa Uhuru kufungwa.

Katibu Mkuu wa klabu ya Simba, Evodius Mtawala, alilidokeza Spoti Starehe kuwa masuala yote mawili hadi sasa hayajafikiwa maamuzi kutokana na kikao hicho kuahirishwa hadi kesho.

Read more...
 
Huondoki- Man City yamuonya Adebayor
Monday, 30 August 2010 05:45

MANCHESTER, England
 
EMMANUEL Adebayor ameeambiwa na Manchester City: "Tunakulipa mishahara yako na utabaki hapa".

Adebayor, mshambulaji kutoka Togo aliyesaini kwa ada ya panuni milioni 25 kutoka Arsenal mwaka jana, anataka kuihama klabu hiyo baada ya kutopangwa katika mechi za mwanzo za Ligi Kuu soka England msimu huu.

"Ikiwa uko kwenye timu na huchezi na klabu nyingine inakutaka ni dhahiri kuwa utakuwa tayari, kwa sababu mimi ni mchezaji na napenda kucheza," alisema Aebayor.

Read more...
 
« StartPrev12345678910NextEnd »

Page 1 of 52

Swali la Leo

"Kitendo cha mabondia wa ngumi za ridhaa kususia mashindano kutokana na kutopatiwa chakura na nauli, ni maamuzi sahihi kwa maslahi ya Taifa letu?"
 

Who's Online

We have 5 guests online

Login Form




Powered by Business Times Ltd Valid XHTML and CSS.